Mkemia Mkuu wa serikali Dk Fidelice Mafumiko amesema ofisi yake haitamvulia mtu yoyote ambaye atabainika kutumia ama kuingiza kemikali nchini bila ya kufuata sheria na taratibu zilizopo kwani madhara ya kemikali yanagusa kizazi hadi kizazi.
Dk Mafumiko ameyasema hayo jijini Dar es salaam wakati alipokutaka na watumiaji wa kemikali hizo nan kutawadharisha kuwa lazima wawe makini wakati wanapozitumia.
Naye Mkurugenzi wa idara ya usimamizi na udhibiti wa kemikali Daniel ndio amesema sheria ipo wazi kuwa mtumiami wa kemikali lazima awe na kibali.
Baadhi ya watumiaji wa kemikali hizo hivyo wamesema wanatambua umuhimu wa kuzitumia na uangalifu japo wanatakiwa kupewa taarifa za mara kwa mara.