Rais Mwinyi akutana na Waziri Nape Zanzibar.

Rais wa Zanzibar Mh. Dk. Hussein Mwinyi amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Habari Mh. Nape Moses Nnauye Ikulu Zanzibar ambapo amempongeza Waziri huyo kwa kupata wadhifa huo huku akimuahidi kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendeleza ushirikiano uliopo ili kuweza kufanikisha kuwapatia wananchi wote mawasiliano.