Back to top

RAIS MWINYI, KIKWETE WATUNUKIWA TUZO

23 March 2023
Share

Rais Zanzibar, Dkt. Hussein Ali Mwinyi na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Kikwete, wametunukiwa Tuzo ya Rais (Presidential Award) ya Mwaka 2023 ,inayotolewa na Taasisi ya Global Water Changemakers, kwa kutambua mchango wao katika kuonesha dhamira ya kweli ya kusimamia na kuleta mabadiliko chanya katika kuendeleza sekta ya maji katika nchi wanazotoka na barani Afrika.
.
Tuzo hizo zimekabidhiwa na  Rais wa Botswana, Mhe.Mokgweetsi Masisi, katika Kongamano la Umoja wa Mataifa kuhusu Maji linaloendelea jijini New York, Marekani.