
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt.Samia Suluhu Hassan, amefanya mabadiliko ya Makatibu Tawala wa Wilaya na Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri za Serikali za Mitaa ambapo katika mabadiliko hayo, Mhe.Rais Samia amefanya uteuzi mpya na kuwahamisha vituo vya kazi baadhi ya Makatibu Tawala na Wakurugenzi Watendaji.

