Back to top

TARI kutoa mbegu za kisasa bure kwa wakulima Nanenane.

31 July 2020
Share

Taasisi ya Utafiti wa Kilimo nchini (TARI) kituo cha Uyole inakusudia kutoa bure mbegu za mazao ya aina mbalimbali kwa wakulima watakaotembelea banda la taasisi hiyo kwenye viwanja vya  maonyesho ya kilimo Nanenane jijini Mbeya.

Afisa Ughani wa TARI kituo cha Uyole, Nyimila Barton Kalindile ameyasema hayo wakati wa maandalizi ya mwisho ya banda la maonyesho la taasisi hiyo kwenye viwanja vya Nanenane vya  John Mwakangale.

Mkurugenzi wa Taasisi hiyo kituo cha Uyole, Dk. Tulole Lugendo Bucheyeki amesema taasisi yake imeongeza idadi za mbegu mpya za mazao ya aina mbalimbali ambazo zitaonyeshwa kwa wananchi kwa mara ya kwanza wakati wa maonyesho ya kilimo ya mwaka huu ambayo yataanza kesho.