
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Khamis Hamza Chillo amewataka viongozi wa mikoa na wilaya nchini kutoa elimu ya upandaji miti kwa wananchi.
Ametaka viongozi hao kwenda kuelimisha wananchi namna bora ya kutunza vyanzo vya maji na kueleza kuwa changamoto kubwa iliyopo kwenye vyanzo hivyo ni shughuli kubwa za kibinadamu.
Naibu Waziri Chillo ametoa kauli hiyo wakati wa ziara ya Kamati ya Mawaziri wa Wizara za Kisekta mkoani Rukwa.
Ameeleza kuwa maeneo mengi yanayovamiwa wavamizi wake hawaendi tu kuvamia bali wanakata na miti na kuharibu vyanzo vya maji ambapo aliwataka viongozi wa mikoa na wilaya kuwaeleza wananchi ambao vijiji vyao vitabaki basi wapande miti.


