Back to top

MENO YA TEMBO NA KIBOKO YAKAMATWA RUVUMA

10 March 2023
Share

Jeshi la Polisi mkoani Ruvuma, limekamata nyara mbalimbali za serikali ikiwemo meno ya tembo mazima 13 na vipande 13, jino moja la kiboko na miiba ya nungunungu.
.
Akitoa Taarifa hiyo, Kamanda wa Polisi mkoani humo, ACP Marco Chilya, amesema Jeshi hilo pia linawashikilia watuhumiwa watatu wa ujangili na silaha tatu zilizotumika kufanya ujangili.