Mkurugenzi Mtendaji ITV/Radio One Joyce Mhavile amepewa tuzo ya heshima katika kukuza, kusimamia,kuendeleza na kutetea tansia ya habari hapa nchini.
"Katika Maisha yetu ambayo Mwenyezi Mungu anatupa kwa upendeleo, kila nafasi unayoipata usiseme hii sio, ukishaanza kuchagua hiki sicho hiki ndicho hutaweza kufikia kile unachokitaka"JoyceMhavile.
Pia amepewa tuzo hiyo kama kioo na mfano wa kuigwa kwa viongozi wanawake wenye uwezo wa hali ya juu kusimamia Tasnia ya habari ndio nchini, na ndio maana akapewa tuzo hiyo ya Malkia wa nguvu mwaka 2018.
Tuzo hiyo ya Malkia wa Nguvu mwaka 2018 imetolewa na Clouds Media Group jijini Dar es Salaam, katika kutambua mchango wa mwanamke mwenye uthubutu na ushawishi.