Back to top

WATUMISHI WA AFYA ZINGATIENI MAADILI

15 September 2023
Share

Mganga mkuu wa serikali, Prof. Tumaini Nagu amewataka watumishi wa Afya kuzingatia maadili katika utoaji wa huduma ikiwemo kutunza siri za wagonjwa.
.
Prof. Nagu amesema hayo akiwa katika ziara ya kukagua utoaji wa huduma katika vituo vya Afya na zahanati kwa ajili ya maandalizi ya uchanjaji wa Polio, mkoani Rukwa.
.
Aidha, Prof. Nagu amewapongeza watumishi wa Zahanati ya Kilimahewa iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga kwa juhudi wanazozionyesha katika kuwahudumia wananchi ikiwa ni pamoja na kumgundua mtoto wenye virusi vya Polio.