Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Prof. Mohammed Ali Sheikh, ametembelea banda la Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA) katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba 2026) yanayoendelea katika Viwanja vya Julius Nyerere, Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kutembelea mabanda ya taasisi zilizo chini ya Wizara.









