Chama cha ACT Wazalendo kinaendelea na vikao vya uteuzi wa mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Zanzibar.
Halmashauri Kuu ya Chama hicho inakaa hii leo katika ukumbi wa Lamada Dar es salaam.
Vikao hivyo vitahitimishwa na Mkutano Mkuu Taifa unaotarajiwa kufanyika Agosti 05, 2020.