Kampuni ya mawasiliano ya Airtel Tanzania imeendelea kupanua huduma zake za kidijitali baada ya kuzindua maduka mawili mapya ya kisasa ya kidijitali katika maeneo ya Tunduma na Mwanjelwa mkoani Mbeya, hatua inayolenga kusogeza karibu huduma za mawasiliano na kifedha kwa wananchi na wafanyabiashara.

