Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Ummy Nderiananga, amewatunuku tuzo ya Shukrani Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bw. Eliakim Maswi kwa kutambua na kuthamini juhudi na mchango wao katika kuhakikisha Watanzania wote wanathaminiwa na kupata Haki zao.