#BURUDANI: Mwanamuziki wa Bongo Fleva, Vanillah amepata shavu katika Kampuni ya Kimataifa ya Apple Music ambapo ameingia katika mpango wao wa kushirikishwa na wasanii wengi wa Kimataifa.
Kupitia Up Next Artist Development Program in East Africa, Vanillah ambaye mbali ya kuimba ni mwandishi wa mashairi atapata shavu la kushirikiana na wasanii kibao wa Kimataifa.
“Najisikia furaha kuwa sehemu ya Apple Music’s Up Next, kwa sababu siyo kila mmoja anaweza kupata bahati kama hii.










