#HABARI: Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo ya Dar es Salaam, imeendelea kusikiliza Ushahidi katika kesi ya Uhaini ya Lissu, ambapo shahidi wa kwanza anaelindwa P2 (38) ambae ni fundi umeme ameshatoa ushahidi wake akiongozwa na Wakili wa Serikali Mkuu Igras Mwinuka.
Ameieleza Mahakama kuwa yeye ni mfuasi wa CHADEMA kuanzia 2021 na alianza kujishughulisha kwenye mikutano na michango ya mikutano tonetone.
Anaeleza kuwa Aprili 4, 2025 alikuwa kwenye shughuli zake Songea anakumbuka kipindi anapitia mtandao wa kijamii alikutana na video ya Lissu, ambapo alikuwa na mkutano Dar es Salaam.
Akiwa kwenye mtandao wa kijamii wa YouTube wakati anaperuzi akakutana na ujumbe wa Mwenyekiti wa chama akiwalekeza kuwa Mwaka huu (mwaka jana 2025) hakutakuwa na uchaguzi, kwa wale ambao wanataka kugombea udiwani, ubunge na Urais wasahau.