Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi, amesema viongozi na Watanzania wanajifunza mengi kutokana na historia ya utendaji kazi wa Mzee John Samwel Malecela, katika nyadhifa mbalimbali alizoshika Serikalini na Chama cha Mapinduzi na ataendelea kuwa hazina muhimu ya maarifa na uzalendo hapa nchini.
Amesema Serikali ina dhamira ya dhati ya kuhakikisha inaweka mazingira rafiki na wezeshi ya ushindani wa haki katika biashara na utoaji huduma , na kuzitaka mamlaka za udhibiti kutekeleza azma hiyo ya serikali.
Mke wa Rais wa Zanzibar, Msarifu ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya wadhamini ya Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation (ZMBF), Mhe.Mama Mariam Mwinyi, amesema Serikali itaendelea kutambua na kuthamini mchango wa Wanawake na kuwashirikisha katika ngazi ya maamuzi na kuendeleza maendeleo nchini.
Serikali za Tanzania na Zambia zimefanikiwa kufuta kero nne kati ya kero 15 zilizokuwepo awali ili kurahisisha michakato ya biashara ya nchi hizo kutegemeana kibiashara........
Jeshi la Polisi, Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, limemkamata Abdulshahib Hegga, maarufu kwa jina la @official_gb64, kwenye mtandao wa Instagram, kwa tuhuma za kuhamasisha watu kufanya vurugu katika mchezo wa Yanga na Simba.....
Jopo la Wataalam kutoka Wizara ya Maji limewasili Nanja ,wilayani Monduli ,mkoa wa Arusha, tayari kwa kuanza kazi ya kujenga bwawa lililobomolewa na maji .