Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, amesema Mashujaa wa Vita ya Majimaji wanapaswa kuenziwa kwa kuimarisha nidhamu ya utendaji kazi, kupinga masuala ya ukabila na kutambua wajibu wa pekee wa kulitetea na kulipigania Taifa.









