Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe Judith Kapinga (Mb.), amesema Serikali itaendelea kuwapa kipaumbele vijana wanaothubutu kuwekeza katika biashara, akimtaja mwanzilishi wa kinywaji cha KIX, kuwa mfano wa vijana wanaopaswa kuungwa mkono kwa kuamini fursa zilizopo nchini.










